MAKALA

 SABABU 4 ZAKUKUFANYA ULE MAYAI

kula yai ni njia rahisi ya kuboresha afya yako.kiini cha yai huwa na madini ya chuma pamoja na kaLshium na ute wa yai huwa na protini za kutosha.madini ya chuma yanasaidia kuongeza damu mwilini na kalshium huimarisha mifupa.kama huna tabia ya kula yai hizi hapa sababu za kwanini ule yai:
1.kupata vitamini
yai moja huwalimejazwa vitamin ambzo ni muhimu kwa afya yako
kwani hufanya kazi mbalimbali kama kuvunja chakula kuwa nguvu za mwili(B2)
kuzalisha seli hai nyekundu za damu(VitaB12)
kuongeza uwezo wa macho kuona (VitA)
inapambana na vichochezi vya kuzalisha kansa(VitE)
kusaidia watoto kukua(Vit A & B2)
2.kusaidia kupunguza uzito
je wajua kama kula yai kunasaidia kupunguza uzito?najua hii itakuchanganya kwakua wengi tunaamini mayai huongeza uzito.lakini utafiti uliofanywa na taasisi ya Rochester Center for Obesity Research imegundua kuwa kula mayai wakati wa asubuhi inaweka ukomo wa kiwango cha uhitaji wa *kalorie kwa siku,kwa zaidi ya kalori 400.
hii ni kweli kwasababu mayai yanakufanya ujiskie umeshiba kwa muda mrefu na hivyo inapelekea wewe kutokula chochote mchana au kati ya asubuhi na mchana.

3.kupata madini muhimu mwilini
mayai huwa yamejazwa madini chuma,zinki na fosforas ambayo ni muhimu sana kwa afya.wanawake wanahitaji sana madini ya chuma kwakuwa hupoteza damu nyingi wakati wa siku zao,ikitokea madini haya yamepungua mara nyingi huwa wanajiskia kuchoka au mwenye harara au hasira (grumpy).Zinki inasaidia kuimarisha kinga mwili pamoja na kusaidia mwili kupata virutubisho kutoka kwenye chakula.fosforasi inasaidia afya ya meno na mifupa.
Na cha ziada ni kwamba kuna madini yanayopatikana kwa kiasi kidogo (trace elements)kama vile seleniam na ayodini.ayodini husaidia kutengeneza homoni,na selenium inasaidia kuondoa uwezekano wa kupata kansa.


4.kupata protini yenye kalori ndogo
yai lenye uzito wa wastani huwalina kalori 70-85 na gramu 6.5 za protini.mwanamke anahitaji gramu 50.
hivyo mayai matatu yatatoa gramu 19.5 karibia nusu ya mahitaji ya siku.(kwa uhakika mahitaji ya protini mwilini hutegemea na uzito na baadhi ya shughuli anazofanya mtu.


*kalori-kizio/kipimo cha joto litolewalo na chakula
...